Tottenham Hotspurs imemsajili golikipa wa Atalanta ya Italia Pierluigi Gollini kwa mkopo wa msimu mzima huku kukiwa na kipengele cha kumnunua mwishoni mwa msimu.
Golloini anakuwa usajili wa kwanza kwa Spurs katika dirisha hili chini ya Nuno Espirityo Santo.
Mlinda mlango huyo alikuwepo kwenye kikosi cha Italia kilichotwaa ubingwa wa Euro 2020.