Home Soka Gomes aipiga mkwara Yanga

Gomes aipiga mkwara Yanga

by Sports Leo
0 comments

Kocha mkuu wa kikosi cha wekundu wa msimbazi Simba sc Mfaransa Didier Gomes ameitahadharisha klabu ya Yanga kujiandaa vizuri kwani wao Simba wamejipanga kulipiza kisasi kwenye mchezo huo wa fainali wa kombe la shirikisho.

Gomes ameyasema hayo alipokuwa akizungumzia maandalizi yao kuelekea mchezo huo wa fainali utakaopigwa mkoani Kigoma tarehe 25 mwezi Julai.

Alisema”matokeo ya mchezo wa Julai 3 yalituumiza sana sisi na mashabiki zetu hivyo tumejipanga kulipa kisasi,tumerekebisha makosa tuliyofanya katika mchezo uliopita na tumeongezea baaadhi ya vitu kwani malengo yetu ni kushinda ubingwa huo”.

banner

Simba na Yanga zitakutana kwa mara kwanza katika fainali za michuano hiyo tangu ianze, na mchezo huo utapigwa katika dimba la Lake Tanganyika mwisho wa reli Kigoma.

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited