Home Soka James kumfuata Xavi Qatar

James kumfuata Xavi Qatar

by Dennis Msotwa
0 comments

Kiungo mshambuliaji wa Everton na timu ya taifa ya Colombia amesafiri hadi katika nchi ya Qatar akiwa na wakala wake kwaajili ya mazungumzo ya kujiunga na Al Saad inayofundishwa na kiungo wa zamani wa Barcelona Xavi Hernandez.

James amepoteza namba katika kikosi cha kwanza tangu kutua kwa kocha Rafael Benitez ambaye anawatumia zaidi Demaray Gray na Aaron Townsend ambao wamesajiliwa msimu huu.

Mchezaji huyo alijiunga Everton mwaka 2020 kwa ushawishi wa aliyekua kocha wa timu hiyo Carlo Ancelotti,na alianza maisha yake vizuri katika klabu hiyo kabla ya majeraha kuharibu kiwango chake.

banner

Kocha wa Al Saad anamtaka kiungo huyo akaungane na kiungo mwingine wa Kihispania Santi Carzola katika safu ya kiungo ya klabu hiyo.

Rodriguez alifanya vizuri katika michuano ya kombe la dunia mwaka 2014 kwa kuibuka kuwa mfungaji bora wa michuano,baada ya michuano hiyo alijiunga na Real Madrid.Baadaye alitolewa kwa mkopo Bayern Munich kabla ya kuuzwa Everton mwaka 2020.

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited