Home Soka Kevin Mbappe Atua Genk

Kevin Mbappe Atua Genk

by Sports Leo
0 comments

Mchezaji kinda wa Kitanzania Kevin John maarufu kama ”Mbappe” amejiunga rasmi na klabu ya KRC Genk ya nchini Ubelgiji akitokea katika akademi ya klabu ya Leicester ya nchini England alikokua akisoma na kupata  mafunzo ya soka.

Mchezaji huyo ametambulishwa rasmi na klabu hiyo ya Ubelgiji baada ya kufikisha miaka 18 inayomruhusu kusajiliwa kama mchezaji wa kulipwa na atajiunga moja kwa moja na timu ya wakubwa tofauti na ilivyoripotiwa awali kuwa angejiunga na timu ya vijana ya Genk.

Katika taarifa ya klabu hiyo imemshukuru Mbwana Samatta kwa kuwapa vidokezo kuhusu kinda huyo ikimtaja kama kama kijana imara na mwenye kasi akisaini hadi mwaka 2024.

banner

 

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited