Timu ya soka ya manispaa ya Kinondoni(Kmc) imemtimua kocha Jackson Mayanja baada ya kuwa na mwenendo usioridhisha hasa uwanjani hususani baada ya kutopata matokeo yasiyorodhisha.
Timu hiyo imekua na mwenendo wa kusuasua tangu ilipoachana na kocha Ettiene Nadyiragije ambaye alijiunga na Azam fc kisha taifa stars ndipo alipoteuliwa mayanja kushika nafasi hiyo na licha ya kutofanikiwa kuingia raundi ya pili ya michuano ya kombe la shirikisho baada ya kutolewa na As kigali ya Rwanda bado aliendelea kupoteza michezo ya ligi kuu ikwemo wa jana dhidi ya Kagera Sugar.
Taarifa rasmi kutoka Kmc imeeleza kuachana na kocha huyo baada ya makubaliano ya pande mbili kufikiwa kwa maslahi mapana ya klabu.
🎯 Usipitwe!
Kuwa wa kwanza kupata habari za moto za michezo nchini Tanzania na duniani kwa ujumla, moja kwa moja kwenye barua pepe yako kutoka SportsLeo Bongo!
- ✅ Matokeo ya mechi
- ✅ Uchambuzi wa kina
- ✅ Habari za ndanii ya timu zako pendwa
✉️ Quality content, no spam. Unsubscribe anytime.