17
Shirikisho la mpira wa miguu barani Afrika (CAF) limewaruhusu wachezaji watatu wa timu ya Taifa ya Uganda Nahodha Dennis Onyango, Farouk Miya na Thadeo Lwanga baada ya majibu ya awali kuonesha wana Covid19 kitu ambacho kilipingwa na Uganda ambao walienda kupima tena kwenye maabara ya SADC na kuonesha wachezaji hawana maambukizi ya Corona.
Baada ya kuonesha hawana maambukizi shirikisho la soka Uganda waliandika barua Caf ikiwaomba wawaruhusu wachezaji hao kucheza mchezo huo dhidi ya Malawi ndio CAF wamewaruhusu wachezaji hao na sasa Onyango na Miya wameanza kikosi cha kwanza huku Lwanga akianzia bechi iwapo Thadeo Lwanga wa Simba ingekuwa kweli ana Covid19 alikuwa anaukosa mchezo wa klabu bingwa dhidi ya As Vita April 03.