Taarifa kutoka nchini Sudan zinadai kocha mkuu wa klabu ya El Merrekh amemuomba tajiri wa klabu hiyo kumsajili golikipa wa klabu ya Simba sc Aishi Manula.
Kocha huyo amevutiwa na uwezo wa kipa huyo tegemea nchini pamoja na timu ya Taifa ya Tanzania kutokana na uhodari wake wa kuokoa michomo uliosaidia kuifanya klabu ya Simba sc kuongoza kundi lake katika michuano ya klabu bingwa barani Afrika hali iliyomfanya kutoruhusu goli mpaka sasa.
Inadaiwa klabu hiyo inajiandaa kutoka kiasi cha dola laki moja kama ofa ya awali kwa klabu ya Simba sc ili kumnasa kipa huyo.