Home Soka Manyama Atua Msimbazi

Manyama Atua Msimbazi

by Sports Leo
0 comments

Beki wa kushoto wa Ruvu Shooting Edward Charles Manyama jana jioni amemalizana na Mabingwa watetezi wa ligi kuu Tanzania Bara Simba SC kwa kusaini kandarasi ya miaka miwili (2) kwa mujibu wa taarifa za ndani za klabu hiyo.

Manyama amekuwa na kiwango bora tangu msimu uliopita na kupata nafasi kwenye kikosi cha timu ya Taifa ya Tanzania (Taifa Stars) huku akishtua wadau wa michezo baada ya kuhama kutoka katika klabu ya Namungo Fc inayoshiriki michuano ya kimataifa na kwenda Jkt Tanzania kwa mkataba wa miezi 6.

Tayari mchezaji huyo alishahusishwa na Yanga sc huku taarifa zikidai kuwa alishamalizana na Yanga sc na ilibaki kusaini tu.

banner

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited