Home Soka Mapro Watano Kutua Yanga sc

Mapro Watano Kutua Yanga sc

by Sports Leo
0 comments

Klabu ya Yanga sc inatarajiwa kusaini wachezaji wa kigeni wapya watano ili kuongeza nguvu katika kikosi hicho kuusaka ubingwa wa ligi kuu msimu ujao.

Mpaka sasa klabu hiyo ina wachezaji wa kigeni tisa huku ikiwa tayari imeachana na Carlos Carlinhos na ina mpango wa kutema wengine watano wakiongozwa na Fiston Abdulrazack pamoja na Michael Sarpong ili kutoa nafasi kwa wengine watano kuingia kikosini.

Inatajwa tayari timu hiyo imemsajili Djuma Shabani huku ikisaka beki wa kati mbadala wa Lamine Moro ambaye majeraha na utovu wa nidhamu vinamponza huku mazungumzo na Heritier Makambo yakiwa yameanza kuongeza nguvu katika upatikanaji wa mabao na kiungo mshambuliaji inadaiwa tayari usajili unaendelea na anatokea nchini Kongo.

banner

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited