Klabu ya Kaizer Chief imethibitisha kumfungashia vilago kocha mkuu Gavin Hunt licha ya kufanikiwa kuivusha timu mpaka hatua ya nusu fainali ya michuano ya klabu bingwa Afrika baada ya kuifunga Simba sc kwa jumla ya mabao 4-3 katika michezo yote miwili.
Makocha wasaidizi Arthur Zwane na Dillon Sheppard watakaimu nafasi hiyo hadi kocha mkuu mpya atakapoteuliwa huku mfululizo wa matokeo yasiyoridhisha na kiwango kibovu cha timu ikiwa kimechangia kutimuliwa kwake.
Takwimu za kocha huyo tangu ajiunge na klabu hiyo katika kipindi cha miezi nane ni alihudumu katika michezo 44 akishinda 12 sare 15 na kufungwa 15 huku akiiacha klabu hiyo katika nafasi ya 11 ya ligi kuu Afrika Kusini.