Home Soka Mbappe: Niliomba kuondoka PSG

Mbappe: Niliomba kuondoka PSG

by Dennis Msotwa
0 comments

Mshambuliaji wa kimataifa wa Ufaransa na klabu ya Paris Saint German amekiambia kituo cha habari za michezo cha RMC cha nchi hiyo kuwa ni kweli aliomba kuondoka klabuni hapo katika dirisha lililopita la usajili la majira ya joto.

Mbappe amesema kuwa aliomba kuondoka mwezi Julai mwaka huu kwasababu kwa kipindi hicho hakutaka kuongeza mkataba mpya wa kuendelea na matajiri hao,hivyo alitaka PSG wapate ada ya uhamisho ili waweze kupata mbadala wake sahihi atakapoondoka.

Aliendelea kusema ”nilitaka kutovunjiana heshima kati yangu na klabu,nikawaambia kama hamtaki niondoke basi sawa nitasalia hapa.Binafsi sikufurahishwa na PSG kusema kuwa nimeomba kuondoka ndani ya wiki ya mwisho ya mwezi Agosti kwasababu si kweli,ilinifanya nijisikie kama mwizi,niliwaambia mapema mwezi Julai na sio kama walivyosema”.

banner

Mchezaji huyo pia amepinga madai kwamba alikataa ofa 7 za kuongeza mkataba kutoka PSG akisema kuwa amekuwa na furaha kwa misimu minne yote aliyoitumikia timu na bado ana furaha licha ya kushindwa kuondoka.

Mbappe anatarajiwa kuondoka bure PSG na kujiunga na Real Madrid ambao ndio klabu pekee iliyoonesha kumhitaji katika dirisha lililopita la usajili.

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited