Aliyekuwa mshambuliaji wa Azam FC, Idriss Mbombo amejiunga na klabu ya Nkana FC ya Zambia na kutambulishwa rasmi kuwa mchezaji wa klabu hiyo kwa mkataba ambao haukuwekwa wazi na kutambulishwa siku ya ijumaa na Mtendaji mkuu wa klabu hiyo Kelvin Mutafu.
Mshambuliaji huyo aliomba kuvunja mkataba wake ambao ulisalia na klabu ya Azam FC ili awe mchezaji huru ambapo muda mchache alisafiri haraka kwenda nchini Zambia kujiunga na Nkana ambapo alijumuika na mastaa wengine watatu katika utambulisho huo.
🎯 Usipitwe!
Kuwa wa kwanza kupata habari za moto za michezo nchini Tanzania na duniani kwa ujumla, moja kwa moja kwenye barua pepe yako kutoka SportsLeo Bongo!
- ✅ Matokeo ya mechi
- ✅ Uchambuzi wa kina
- ✅ Habari za ndanii ya timu zako pendwa
✉️ Quality content, no spam. Unsubscribe anytime.
Mshambuliaji huyo ameondoka Azam Fc baada ya kukosa nafasi katika kikosi cha kwanza ambapo kocha Yousouph Dabo anapenda zaidi kumtumia Prince Dube kama mshambuliaji wake wa kati huku akisaidiwa na Allasane Diara na mara nyingi Mbombo hukaa jukwaani.