Home Soka Mcolombia Atambulishwa Azam Fc

Mcolombia Atambulishwa Azam Fc

by Sports Leo
0 comments

Klabu ya soka ya Azam Fc imemtambulisha mshambuliaji Franklin Navarro raia wa Columbia mwenye miaka 24 ambaye amejiunga na klabu hiyo kwa mkataba wa miaka miwili akitokea klabu ya Cortuluá ya nchini humo.

Usajili wa mshambuliaji huyo unaweka rekodi ya kuwa Mcolombia wa kwanza kucheza nchini ambapo anatarajiwa kuchukua nafasi ya Idriss Mbombo ambaye kwa mujibu wa taarifa za ndani ni kuwa anaweza kutemwa muda wowote klabuni hapo.

Azam Fc tayari imemtambulisha mshambuliaji huyo kupitia vyanzo rasmi vya taarifa vya klabu hiyo na tayari amejiunga na kambi ya timu hiyo iliyoko visiwani Zanzibar katika michuano ya kombe la Mapinduzi ambapo jioni hii wamecheza na Mlandege Fc na kutoa suluhu.

banner

Mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 24, inaelezwa ni mtalamu wa kucheka na nyavu na ana kasi ya kukimbia huku akiwa na uwezo wa kucheza kama mshambuliaji wa kati ama pembeni.

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited