Home Soka Miquissone kutua Al Ahly

Miquissone kutua Al Ahly

by Sports Leo
0 comments

Mshambuliaji wa Simba na timu ya Taifa ya Msumbiji Luis Miquissone huenda akajiunga na mabingwa wa klabu bingwa Afrika Al Ahly ya Misri.

Al Ahly wameonesha nia ya dhati kumnunua mchezaji huyo ambaye anahitajika sana na rais wa klabu hiyo Mahmoud El Khatib na wako tayari kupeleka ofa inayokadiriwa kuanzia bilioni mbili za Kitanzania ambayo wanaamini itatosha kumnasa Mmakonde huyo.

Mchezaji huyo pia alikuwa anahitajika na klabu ya Kaizer Chiefs ya Afrika Kusini,lakini wamejitoa baada ya kusikia ofa ya Al Ahly kwani wao hawako tayari kulipa kiasi wanachotaka kutoa Wamisri hao.

banner

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited