Home Soka Mkude Yupo Sana Msimbazi

Mkude Yupo Sana Msimbazi

by Dennis Msotwa
0 comments

Licha ya kuwa na matatizo ya kinidhamu ya mara kwa mara kiasi cha kuitwa katika kamati ya nidhamu ya klabu ya Simba sc,Inadaiwa kuwa kiungo wa klabu hiyo Jonas Mkude bado yupo sana klabuni hapo.

Hivi majuzi kamati ya nidhamu ya klabu hiyo iliamuru kuwa staa huyo aende kupimwa akili katika Hospitali ya taifa ya Muhimbili kutokana na mfululizo wa matukio hayo ili kujua aina ya uamuzi wa kuchukua kwa kamati hiyo baada ya kupata ripoti ya madaktari.

Mkuu wa kamati hiyo Seleman Kova amethibitisha kuwa staa huyo ana mkataba na klabu hiyo hivyo hawafanyi kwa lengo la kutaka kumkomoa ama kumuacha mchezaji huyo.

banner

“Kuna watu nimeskia katika maoni yao wanafikiria labda mkataba wa Mkude unakaribia kuisha kwa hiyo Simba au sisi tunatumika kumkomoa mchezaji.

“Nimeangalia mkataba wa Mkude bado ni mbichi kabisa, ni mchezaji anayependwa na kila Mwanasimba lakini linapotokea tatizo ni lazima lishughukikiwe.Alisema Kamanda Kova aliyewahi kuwa mkuu wa polisi mkoa wa Dar es saalam.

 

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited