Home Soka Morocco yaifuata Cameroon 16 Bora

Morocco yaifuata Cameroon 16 Bora

by Dennis Msotwa
0 comments

Timu ya Taifa ya Morocco maarufu kama simba wa Atlas wamefanikiwa kusonga mbele katika hatua ya mtoano ya michuano ya kombe la Mataifa Afrika(AFCON) linaloendelea nchini Cameroon.

Morocco wamefanikiwa baada ya kuifunga timu ya Taifa ya Visiwa vya Comoro kwa mabao 2-0 na kufikia alama sita kileleni mwa msimamo wa kundi C na hivyo kujihakikishia nafasi.

Magoli kutoka kwa washambuliaji Selim Amallah dakika ya 16 na Zakaria Aboukhlal dakika ya 89 yalitosha kuwapa ushindi muhimu huku mshambuliaji Yousuf En Nesyri akikosa mkwaju wa penati dakika ya 83.

banner

Kwa upande mwingine timu ya Taifa ya Ghana imeshindwa kupata ushindi katika mchezo wake wa pili katika kundi hilo baada ya sare ya 1-1 na Gabon na kuwaweka katika nafasi finyu ya kufuzu hatua ya mtoano.

Nayo timu ya Taifa ya Malawi anayochezea mchezaji wa Simba sc Peter Banda imeapa ushindi wa 2-0 dhidi ya Zimbabwe katika mchezo wa kundi B.

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited