Home Soka Morrison,Metacha Wabaki Dar

Morrison,Metacha Wabaki Dar

by Dennis Msotwa
0 comments

Mastaa tegemeo katika kikosi cha Yanga Kipa Metacha Mnata na Winga Benard Morrison wameachwa katika kikosi cha timu hiyo kilichoondoka leo kuelekea Shinyanga kuwavaa Mwadui fc.

Yanga imeondoka leo jijini Dar es salaam kwa usafiri wa basi na kuwaacha mastaa hao kwa sababu mbalimbali ambapo Morrison alichelewa msafara wa timu huku Metacha akiwa na ruhusa maalumu kutoka kwa uongozi kushughulikia matatizo ya kifamilia.

Taarifa kutoka Yanga zinadai mastaa hao wataungana na timu hiyo kesho ambapo wataondoka kwa ndege wakiwa na kocha Luc Eymael anayetarajiwa kuwasili leo saa saba mchana.

banner

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited