Home Soka Mourinho Atimuliwa Tena

Mourinho Atimuliwa Tena

by Dennis Msotwa
0 comments

Klabu ya Tottenham imemfuta kazi mkufunzi wake mkuu Jose Mourinho baada ya kudumu nae kwa miezi 17 tangu ajiunge mwaka 2019 akisaidia timu kumaliza nafasi ya sita ya ligi kuu msimu uliopita.

Pamoja na Mourinho,Pia wasaidizi wake wote wametimuliwa klabuni hapo wakiwemo kocha ya viungo,makipa na kocha wa kikosi cha kwanza wakiiachia timu hiyo kibarua kizito dhidi ya Man city katika mchezo wa fainali ya Carabao Cup tarehe 25 mwezi huu.

Mourinho amevuna alama mbili pekee katika mechi tatu za ligi kuu nchini Uingereza huku akitolewa katika michuano ya Europa huku akifungwa michezo kumi katika msimu huu tangu aanze kufundisha soka.

banner

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited