Home Soka Msiba Wamzuia Ninja Dar

Msiba Wamzuia Ninja Dar

by Dennis Msotwa
0 comments

Beki wa klabu ya Yanga sc Abdala Shaibu ”Ninja”leo anatarajiwa kusafiri kuungana na timun hiyo jijini Mbeya baada ya kutokusafiri jana kufuatia kupatwa na msiba wa dada yake siku ya juzi.

Beki huyo katili alipata taarifa za msiba wa dada yake wakati timu ikiwa katika maandalizi ya kuwavaa Azam Fc na ndipo alipoamua kumaliza mechi kisha kuhudhuria mazishi ya dada yake yaliyofanyika jana.

Hata hivyo baada ya msafara wa klabu hiyo kusafiri hapo jana kuelekea jijini Mbeya ambapo wataweka kituo kabla ya kuelekea mjini Sumbawanga kuwavaa Prisons siku ya ijumaa jioni ambapo beki huyo atakuwepo baada ya kukamilisha taratibu zote za safari na leo jioni ataungana na wenzake mazoezini.

banner

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited