Home Soka Namungo Yatoa Dozi Nene

Namungo Yatoa Dozi Nene

by Sports Leo
0 comments

Klabu ya Namungo Fc imefanikiwa kuibuka na ushindi wa magoli 6-2 dhidi ya Primera de Augosto katika mchezo wa kombe la shirikisho barani Afrika uliofanyika katika uwanja wa chamazi jijini Dar es salaam. 
Magoli ya Namungo yamefungwa na Hashim Manyanya (32’), Sixtus Sabilo (38’, 59’), Reliants Lusajo (55’), Erick Kwizera 66’ na Stephen Sey dakika ya 72.
Mechi ya marudiano itapigwa ndani ya saa 72 zijazo, na Namungo itahitaji sare au kufungwa si zaidi ya mabao 4-0 ili kuingia hatua ya makundi ya michuano hii ya Kombe la Shirikisho barani Afrika.
Awali mchezo huo ilibidi uchezwe nchini Angola lakini changamoto ya ugonjwa wa Corona ilisababishwa mchezo huo kuahirishwa na kuamuliwa kufanyika nchini kwa michezo yote miwili.

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited