Home Soka Ninja,Carlinhos Kuwakosa Namungo Fc

Ninja,Carlinhos Kuwakosa Namungo Fc

by Dennis Msotwa
0 comments

Klabu ya Yanga sc itawakosa wachezaji wake sita kuelekea katika mchezo wa ligi kuu dhidi ya Namungo Fc utakaofanyika siku ya jumamosi katika uwanja wa Majaliwa mjini Ruangwa kutokana na sababu mbalimbali.

Farid Musa,Carlos Carlinhos,Haruna Niyonzima,Balama Mapinduzi wote wakisumbuliwa na majeruhi mbalimbali pamoja na kukosa utimamu wa mwili kuelekea mchezo huo huku Abdalla Shaibu Ninja na Yassin Mustapha nao wakiwa wanamalizia matibabu yao ya mwisho.

Tayari kikosi cha Yanga sc kimeondoka jijini Dar es salaam na kuweka kambi katika mkoa wa Mtwara kujiandaa na mchezo huo mkali wakijiandaa kutua Ruangwa siku ya Ijumaa.

banner

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited