Home Soka Pirlo wa Leeds atakiwa Man Utd

Pirlo wa Leeds atakiwa Man Utd

by Sports Leo
0 comments

Manchester united ipo katika mpango wa kumsajili kiungo mkabaji wa Leeds united Kavin Phillips baada ya kushindwa kumsajili kiungo wa West ham Declan Rice kutokana na dau kubwa lililowekwa na klabu yake.

Kavin amekuwa katika kiwango kizuri chini ya mkufunzi Marcelo Bielsa tangu kupanda kwa Leeds katika ligi kuu ya Uingereza msimu uliopita kiasi cha kumfanya kocha wa timu ya taifa Gareth Southampton kumjumuisha katika timu ya taifa na kuwa tegemeo kwenye timu hiyo.

Manchester united wamekuwa wakisaka kiungo mkabaji kwa muda mrefu baada ya Fred na McTominay kushindwa kuonesha ubora katika eneo hilo huku Leeds united wakihitaji kiasi cha Euro milioni 60 kufanya biashara.

banner

Mpango huo umekuja baada ya West ham kuhitaji dau la Euro milioni 100 kumuachia Rice kiasi ambacho Man utd wanaona hawako tayari kukitoa,hivyo kumgeukia Muingereza mwezake Phillips anayefananishwa na gwiji wa zamani wa Italia Andrea Pirlo kutokana  na uchezaji wake.

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited