Kiungo wa manchester united Paul Pogba amezua balaa klabuni hapo baada ya uongozi kuamua kuweka dau la Paundi 180m kwa timu ambayo itamuhitaji staa huyo.
Imeripotiwa kuwa united imeweka dau hilo ili kuzuia dili la mchezaji huyo kujiunga na Real madrid na Juventus ambazo zinamnyemelea kwa kasi mfaransa huyo.
Pogba 26 tayari amesharipoti katika kambi ya mazoezi ya klabu hiyo iliyopo barani asia kujindaa na msimu mpya wa ligi kuu nchini humo ambapo msimu uliopita timu hiyo ilikosa nafasi ya kumaliza nne bora na kushindwa kupata nafasi ya kushiriki michuano ya klabu bingwa barani ulaya.
🎯 Usipitwe!
Kuwa wa kwanza kupata habari za moto za michezo nchini Tanzania na duniani kwa ujumla, moja kwa moja kwenye barua pepe yako kutoka SportsLeo Bongo!
- ✅ Matokeo ya mechi
- ✅ Uchambuzi wa kina
- ✅ Habari za ndanii ya timu zako pendwa
✉️ Quality content, no spam. Unsubscribe anytime.