Timu ya Prisons imefanikiwa kulazimisha suluhu na Simba sc katika mchezo uliomalizika jioni hii katika uwanja wa uhuru jijini Dar es salaam.
Mchezo ulioanza kwa kasi ukitawaliwa na krosi nyingi kuelekea langoni mwa Prisons ulimalizika kwa matokeo hayo baada ya mabeki wa timu hiyo kufanikiwa kuwadhibiti Meddie Kagere na Miraji Athuman huku Cletous Chama na Shiboub wakikosa ubunifu wa kupenyeza mpira langoni mwa wajelajela hao.
Kwa matokeo hayo bado Simba wanaendelea kuongoza ligi wakiwa na pointi 22 huku prisons akipanda mpaka nafasi ya pili akiwa na pointi 19 baada ya kucheza michezo 11.
🎯 Usipitwe!
Kuwa wa kwanza kupata habari za moto za michezo nchini Tanzania na duniani kwa ujumla, moja kwa moja kwenye barua pepe yako kutoka SportsLeo Bongo!
- ✅ Matokeo ya mechi
- ✅ Uchambuzi wa kina
- ✅ Habari za ndanii ya timu zako pendwa
✉️ Quality content, no spam. Unsubscribe anytime.