Home Soka Ronaldo Kurudi Man United

Ronaldo Kurudi Man United

by Dennis Msotwa
0 comments

Simu moja tu ya Sir Alex Ferguson imebadili uelekeo wa Cristiano Ronaldo aliyekua mbioni kuelekea Manchester City kujiunga na klabu hiyo na kuamua kujiunga na Manchester United iliyochini ya Olle Gunnar Solskjaer huku akiungana na mastaa kama Paul Pogba na Bruno Fernandes pamoja na Edson Cavani.

Awali Ronaldo alionyesha nia ya kuondoka Juventus ambayo ilihitaji paundi milioni 30 kumuachia staa huyo ambaye naye alikubali kujiunga na Man City iliyoonyesha nia ya kumsajili mshambuliaji huyo mwenye miaka 36 huku ikimuandalia mshahara wa paundi laki tano kwa wiki lakini kuingia kwa Man united kwenye dili hilo dakika za mwishoni kulibadilisha upepo na staa huyo sasa atatua Man United baada ya kukubali mapendekezo ya mkataba wa Man united ambao pia watailipa Juventus kiasi cha paundi 25 milioni.

Inadaiwa Ronaldo amekubali mshahara wa kiasi cha paundi 375000 kwa wiki akiacha mshahara mnono ambao angelipwa na Man city huku ikidaiwa simu ya Ferguson kwa mama wa mchezaji huyo ilibadili kila kitu na kumfanya staa huyo arudi Man united alipoondoka miaka 12 iliyopita ambapo alidumu klabuni hapo kwa miaka 6 akishinda mataji mbalimbali ikiwemo Epl mara tatu.

banner

Man united inasemekana ina mpango wa kuwatoa kwa mkopo Anthony Martial kwenda Real Madrid ambayo itamlipa mshahara wote pamoja na Jesse Lingard kwenda Westham United ili kufidia kiasi cha mshahara wa Ronaldo klabuni hapo.

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited