Mlinzi wa kati wa Chelsea Antonio Rudiger ameanza kuiweka mashakani klabu yake juu ya mustakabali wake mara baada ya kuanza kuhusishwa na vilabu vikubwa barani Ulaya kama Paris Saint German,Real Madrid na Bayern Munich.
Rudiger yupo ndani ya msimu wa mwisho darajani na mazungumzo ya mkataba mpya kati yake na waajiri wake hao.
Beki huyo amekuwa katika kiwango bora tangu kuajiriwa kwa kocha Thomas Tuchel katika viunga vya Stamford Bridge,kabla ya hapo alikuwa katika wakati mgumu chini ya Frank Lampard mpaka kuhusishwa na kuuzwa.
🎯 Usipitwe!
Kuwa wa kwanza kupata habari za moto za michezo nchini Tanzania na duniani kwa ujumla, moja kwa moja kwenye barua pepe yako kutoka SportsLeo Bongo!
- ✅ Matokeo ya mechi
- ✅ Uchambuzi wa kina
- ✅ Habari za ndanii ya timu zako pendwa
✉️ Quality content, no spam. Unsubscribe anytime.
Chelsea sasa watapaswa kuongeza juhudi za kumshawishi beki huyo kubaki na inasemekana ni harakati za wakala wake katika kumtafutia mteja wake mkataba mnono kwani mkataba wake unaisha Juni 2022.