Home Soka Rudiger aiweka njia panda Chelsea

Rudiger aiweka njia panda Chelsea

by Dennis Msotwa
0 comments

Mlinzi wa kati wa Chelsea Antonio Rudiger ameanza kuiweka mashakani klabu yake juu ya mustakabali wake mara baada ya kuanza kuhusishwa na vilabu vikubwa barani Ulaya kama Paris Saint German,Real Madrid na Bayern Munich.

Rudiger yupo ndani ya msimu wa mwisho darajani na mazungumzo ya mkataba mpya kati yake na waajiri wake hao.

Beki huyo amekuwa katika kiwango bora tangu kuajiriwa kwa kocha Thomas Tuchel katika viunga vya Stamford Bridge,kabla ya hapo alikuwa katika wakati mgumu chini ya Frank Lampard mpaka kuhusishwa na kuuzwa.

banner

Chelsea sasa watapaswa kuongeza juhudi za kumshawishi beki huyo kubaki na inasemekana ni harakati za wakala wake katika kumtafutia mteja wake mkataba mnono kwani mkataba wake unaisha Juni 2022.

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited