Home Soka Sancho Kutua United Baada ya Euro

Sancho Kutua United Baada ya Euro

by Dennis Msotwa
0 comments

Klabu za Man United na Borrussia Dortmund zimekubaliana kimsingi kuuziana mcheza Jadon Sancho kwa kiasi cha paundi 73M ambapo mchezaji huyo atajiunga na Man utd baada ya kukamilisha taratibu za kiafya.

Katika dili hilo klabu ya Man city itafaidika na mauzo ya mchezaji huyo kwa maana ndio klabu iliyomkuza katika akademi kabla ya kujiunga na Dortmund.

Kwa muda mrefu timu hizo zimekua na majadiliano kuhusu kuuziana mchezaji huyo lakini bei iliyowekwa na Dortmund ilikua kikwazo kwa Man united huku ikisemekana tayari mchezaji alishaonesha nia ya kujiunga na mashetani wekundu wakiwa tayari wameshakubalina mpaka maslahi binafsi huku akiwa na mkataba mfupi uliosalia klabuni hapo.

banner

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited