Home Soka Shangwe Lamponza Kocha Miembeni

Shangwe Lamponza Kocha Miembeni

by Sports Leo
0 comments

Shirikisho la Mpira wa Miguu Zanzibar (ZFF) limemfungia miezi sita na kumpiga faini ya Tsh. 500,000 Kocha wa timu ya Miembeni, Suleiman Mohamed kwa utovu wa nidhamu.

Kocha huyo alishangilia kwa kushusha suruali chini na kubaki na nguo ya ndani mbele ya mashabiki baada timu yake kushinda bao 1-0

Adhabu hiyo iliyosainiwa na Katibu wa Kamati ya Mashindano ya ZFF, Hussein Ahmada, ni kwa mujibu kifungu namba 31 cha kanuni ya kuendesha mashindano hayo.

banner

Hussein alisema Kocha huyo atatakiwa kulipa faini hiyo ndani ya kipindi anachotumikia adhabu hiyo na akishindwa kulipa faini adhabu itaendelea mara mbili.

Credit:Jami Forums

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited