Home Soka Simba SC waachia jezi mpya

Simba SC waachia jezi mpya

by Sports Leo
0 comments

Mabingwa wa soka Tanzania Bara klabu ya soka ya Simba imelazimika kuachia jezi mpya zitakazotumika kwaajili ya michuano mbalimbali itayoshiriki timu hiyo kwa msimu wa 2021/2022 baada ya kuvuja kwa jezi hizo.

Awali uzinduzi rasmi wa jezi hizo ulitarajiwa kufanyika kesho Jumamosi Septemba 4 lakini wamelazimika kuziachia jezi hizo hii leo kwa kile wanachodai ni presha kubwa kutoka kwa mashabiki kuzihitaji jezi hizo.

Kaimu Afisa habari wa Simba SC Ezekiel Kamwaga amesema kuwa ”mashabiki wanahitaji sana jezi,uongozi umeona hauwezi tena kusubiri,presha ni kubwa sana.Sasa rasmi jezi za Simba zinapatikana leo kwenye maduka yote ya VUNJABEI.Uzinduzi uko palepale kesho”.

banner

Katika hatua nyingine kuthibitisha kuvuja kwa jezi hizo Kamwaga amesema ”kuna timu kama Coastal Union wametoa jezi lakini hazikuvuja,imefika Simba jezi imevija.Hii ni tabia mbaya,kwanini uvujishe jezi ya timu?tukianza utani wa jadi wa kuvujishana jezi tunapokwenda itakuwa ni vita”.

Simba wameachia jezi za aina nne ambazo ni ya nyumbani(nyekundu),ugenini(nyeupe),ya tatu(nyeusi) na casual.

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited