Klabu ya soka ya Simba imetambulisha mascot ambao watakuwa wakitumika katika michezo ya nyumbani kuleta hamasa na burudani kwa mashabiki wa timu hiyo watakaokuwa wakihudhuria michezo hiyo.
Simba imekuwa klabu ya kwanza nchini kutambulisha mascot kama zifanyavyo klabu mbalimbali duniani.
Mascot huwa ni watu maalumu ambao huvaa vinyago vinavyoendana na taswira au sura ya klabu husika.Klabu mbalimbali kubwa duniani zimekuwa na mascot kwa miaka mingi mfano Manchester United ya England yenye mascot maarufu ajulikanaye kama ‘Fred The Red’.
Huu unatajwa kama ubunifu kwa Simba katika kuelekea tamasha la Simba day ambapo mascot hao watatambulishwa rasmi kwa wanachama,mashabiki na wapenzi wa klabu hiyo yenye makao yake mtaa wa Msimbazi.
🎯 Usipitwe!
Kuwa wa kwanza kupata habari za moto za michezo nchini Tanzania na duniani kwa ujumla, moja kwa moja kwenye barua pepe yako kutoka SportsLeo Bongo!
- ✅ Matokeo ya mechi
- ✅ Uchambuzi wa kina
- ✅ Habari za ndanii ya timu zako pendwa
✉️ Quality content, no spam. Unsubscribe anytime.
Simba SC kwasasa ipo katika wiki ya Simba ambapo shughuli mbalimbali zimeendelea kufanyika kuelekea kilele chake siku ya Jumapili tarehe 19 Septemba katika uwanja wa Benjamin Mkapa Dar es salaam.