Home Soka Simba sc Yawazuia Job,Feitoto Kujiunga U23

Simba sc Yawazuia Job,Feitoto Kujiunga U23

by Dennis Msotwa
0 comments

Kocha mkuu wa timu ya Tanzania kwa vijana wasiozidi umri wa miaka 23 Kim Poulsen ameeleza kuwa alipanga kuwaita wachezaji wa Yanga, Feisal Salum na Dickson Job kikosini kwake lakini imeshindikana kutokana na nyota hao kuwa na ratiba ngumu.

“Nilipanga kuwajumuisha Feisal na Job, lakini wanakabiliwa na mchezo wa fainali hivyo nimewaacha na nimechagua wengine ambao naamini wataiwakilisha nchi vyema,” amesema Kim.

Sambamba na hao kocha Kim alimhitaji kipa wa Mwadui Mussa Mbissa, kwenye kikosi chake lakini imeshindikana kutokana na kuchelewa kwa upatikanaji wa baadhi ya nyaraka zake za kusafiria ikiwemo ‘Visa’ hivyo kumuita Daniel Mgore wa Biashara United.

banner

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited