Home Soka Sven Aibua Mapya Simba sc

Sven Aibua Mapya Simba sc

by Sports Leo
0 comments

Taarifa zinadai aliyekua kocha wa klabu ya Simba sc Sven Vandebroek ameishitaki klabu hiyo katika shirikisho la soka duniani(Fifa) baada ya kutomlipa baadhi ya stahiki zake ikiwemo bonasi za ushindi kwa mujibu wa mkataba wake.

Sven aliyeikacha Simba sc baada ya kufanikiwa kuivusha klabu hiyo amepeleka malalamiko hayo kufuatia kuahidiwa kulipwa mara kadhaa lakini haikua hivyo huku akidai baadhi ya fedha za mishahara pamoja na bonasi za ushindi wa taji la ligi kuu msimu wa 2019/2020.

Pia taarifa zinadai licha ya sababu hiyo pia kulikua na suala la kumpangia kikosi kwa viongozi kulazimisha Meddie Kagere aanze pamoja na mshambuliaji mwingine mfumo ambao kocha huyo hakuwa akiukubali hivyo kumlazimu kuachana na klabu hiyo.

banner

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited