Site icon Sports Leo

Tanzania Yafuzu Afcon ya Ufukweni

Timu ya Taifa ya Tanzania ya soka la Ufukweni imefuzu Fainali za Kombe la Mataifa ya Afrika (Afcon) baada ya ushindi wa jumla wa mabao 12-9 dhidi ya Burundi katika michezo yote iliyochezwa katika fukwe za Coco Dar es salaam.

Licha ya leo Tanzania kufungwa mabao 6-4 katika mchezo wa marudiano lakini ushindi wa mabao 8-3 katika mchezo wa kwanza umewabeba Tanzania.

Exit mobile version