Home Soka Tsh 10,000 tu kuiona Simba vs Yanga ngao ya hisani

Tsh 10,000 tu kuiona Simba vs Yanga ngao ya hisani

by Sports Leo
0 comments

Shirikisho la mpira wa miguu nchini (TFF) limetoa viingilio vya mchezo wa ngao ya hisani baina ya Simba na Yanga unaotarajiwa kufanyika Septemba 25 katika dimba la Benjamin Mkapa Dar es salaam.

Mchezo huo ni kuashiria ufunguzi wa ligi kuu soka Tanzania Bara inayotarajiwa kuanza Septemba 27 mwaka huu.

Kwa kawaida mechi ya ngao ya hisani husimamiwa na TFF tofauti na ligi kuu ambayo husimamiwa na bodi ya ligi,mechi hii huwakutanisha bingwa wa ligi kuu soka Bara na mshindi wa kombe la shirikisho la azam,na iwapo bingwa wa kombe la shirikisho ndiye bingwa wa ligi basi hukutana na mshindi wa pili kwenye msimamo wa ligi kuu.

banner

Simba SC ndio mabingwa wa ligi kuu na kombe la shirikisho msimu wa 2020/2021,hivyo atakutano na Yanga SC waliomaliza nafasi ya pili katika ligi katika mtanange mkali ukizingatia timu zote zimepoteza wikiendi iliyopita hivyo zitapambana kurejesha imani na furaha ya mashabiki wao

Viingilio hivyo ni kama inavyoonekana hapo chini:

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited