Home Soka Uingereza yaitupa nje Ujerumani euro 2020

Uingereza yaitupa nje Ujerumani euro 2020

by Sports Leo
0 comments

Timu ya Taifa ya Uingereza imefuzu kwenda robo fainali ya michuano ya euro baada ya kuichapa timu ya Taifa ya Ujerumani kwa mabao 2-0 katika mchezo wa mtoano uliofanyika katika la Wembley.

Uingereza ilijipatia bao la kwanza dakika ya 75 kupitia Raheem Sterling akipokea pasi ya Luke Shaw, na iliongeza bao la pili dakika ya 85 kupitia nahodha wake Harry Kane akimalizia kwa kichwa krosi ya Jack Grealish.

Hii ni mara ya kwanza kwa Uingereza kuifunga Ujerumani katika hatua za mtoano baada ya miaka 55.

banner

Uingerza sasa itamsubiri mshindi kati ya Ukraine na Sweden katika hatua ya robo fainali ya michuano hiyo inayowashangaza wengi baada ya kuondolewa kwa vigogo watatu Ufaransa,Ureno na Ujerumani waliokuwa kundi moja.

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited