Home Soka Van Gaal arejea Uholanzi

Van Gaal arejea Uholanzi

by Sports Leo
0 comments

Mkufunzi wa soka Luis Van Gaal amerejea tena kuifundisha timu ya taifa ya Uholanzi kwa mara ya tatu baada ya kile cha 2000-2002 na 2012-2014 katika michuano ya kombe la dunia.

Kocha huyo amechukua mikoba ya Frank De Boer aliyechemsha na timu hiyo kwenye michuano ya Euro 2020 na amekuwa bila ya kazi tyangu mwaka 2016 alipofukuzwa na Man Utd.

LVG amesema ‘ni heshima kurejea tena kuifundisha na Uholanzi,soka la Uholanzi siku zote limekuwa moyoni mwangu na timu ya Taifa ni ufunguo wa kulipeleka mbele soka letu’.

banner

Van Gaal amepewa jukumu la kuipeleka Uholanzi kombe la dunia 2022 nchini Qatar pamoja na kuiongoza timu hiyo kwenye michuano hiyo.

 

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited