Bodi ya ligi nchini TPLB imetangaza rasmi kuwa mchezo wa ligi kuu nchini baina ya Yanga sc dhidi ya Simba sc utachezeshwa na waamuzi sita ili kuleta ufanisi zaidi.
Akizungumza na waandishi wa habari katika uwanja wa Benjamini Mkapa katika mkutano maalumu na wanahabari mtendaji mkuu wa TPLB Almas Kazongo alisema kuwa wao kama wasimamizi wa mchezo huo wameona inafaa kutumia waamuzi sita ambapo wanne watakua kama ilivyo mechi zingine huku wale wawili watakaoongezeka watakua nyuma ya magoli.
Mchezo huo wa kusisimua unatarajiwa kufanyika Novemba 7 siku ya jumamosi katika uwanja wa Benjamini Mkapa jijini Dar es salaam ambapo katika mchezo wa mwisho timu hizo kukutana Yanga alifungwa mabao 4-0.
🎯 Usipitwe!
Kuwa wa kwanza kupata habari za moto za michezo nchini Tanzania na duniani kwa ujumla, moja kwa moja kwenye barua pepe yako kutoka SportsLeo Bongo!
- ✅ Matokeo ya mechi
- ✅ Uchambuzi wa kina
- ✅ Habari za ndanii ya timu zako pendwa
✉️ Quality content, no spam. Unsubscribe anytime.