Home Soka Wenger Aula Fifa

Wenger Aula Fifa

by Sports Leo
0 comments

Kocha wa zamani wa klabu ya Arsenal Arsene Wenger ameteuliwa kuwa mkurugenzi wa maendeleo ya soka duniani na shirikisho la mpira duniani(Fifa) na kumaliza tetesi zilizoenea kuwa atajiunga na klabu ya Bayern Munchen ya Ujerumani.

Kocha huyo aliyeifundisha Arsenal kwa miaka 22 na kuisaidia kuchukua ubingwa na ligi mara tatu ameteuliwa baada ya kukaa bila kujihusisha moja kwa moja na mpira tangu aondoke klabuni hapo mwezi may mwaka jana.

“Naangalia mbele zaidi kuchukua changamoto hii muhimu duniani” alisema kocha wakati akihojiwa na shirika la habari la Bbc.

banner

Kocha huyo baada ya kuchukua nafasi hiyo atajihusisha zaidi na maendeleo ya mpira kwa wanaume na wanawake pamoja na masuala ya kiufundi duniani.

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited