Mtendaji mkuu wa Manchester United Ed Woodward ataendelea na kushikiria nafasi hiyo hadi pale atakapokamilisha mchakato wa kupata kocha wa muda na baadae kocha wa kudumu ndani ya klabu hiyo.
Mkataba wake ulikuwa unaisha mwishoni mwa mwaka huu lakini wamiliki wanataka abakie akamilishe kwanza zoezi hilo.
Man Utd ilisitisha mkataba wa kocha wake mkuu Ole Gunnar Solskjaer siku ya Jumapili na kumpa majukumu ya kukaimu nafsi hiyo Michael Carrick ambaye alikua kocha msaidizi.
Majina kama Laurent Blanc,Carrick mwenyewe,Ralf Rangnick wanatajwa kuwania nafasi ya kocha wa muda mpaka mwishoni mwa msimu huu huku Mauricio Pochettino,Zinedine Zidane na Eric Ten Haag wakitajwa kuchukua majukumu ya kocha mkuu msimu utakapotamatika.
🎯 Usipitwe!
Kuwa wa kwanza kupata habari za moto za michezo nchini Tanzania na duniani kwa ujumla, moja kwa moja kwenye barua pepe yako kutoka SportsLeo Bongo!
- ✅ Matokeo ya mechi
- ✅ Uchambuzi wa kina
- ✅ Habari za ndanii ya timu zako pendwa
✉️ Quality content, no spam. Unsubscribe anytime.
Hata Pochettino ndiye chaguo la kwanza la bodi ya Manchester United kuchukua mikoba ya Ole,huku kocha huyo wa sasa wa PSG akionesha nia ya kurejea Uingereza.