Klabu ya Yanga sc inakusudia kukata rufaa kupiga adhabu aliyopewa makamu mwenyekiti wa klabu hiyo Fredrick Mwakalebela ya kufungiwa kutojihusisha na soka kwa miaka mitano pamoja na faini ya shilingi milioni 7 za kitanzania.
Mkuu wa Idara ya Habari ya klabu hiyo Hassan Bumbuli alithibitisha kuhusu suala hilo ambapo wanasubiri nakala ya hukumu ili kukata rufaa.
“Tumechelewa kukata rufaa kwa kuwa tulikuwa tunasubiri muongozo wa TFF, lakini kama klabu hatujakubaliana na adhabu hiyo kwa makamu mwenyekiti wetu,” amesema Bumbuli.
🎯 Usipitwe!
Kuwa wa kwanza kupata habari za moto za michezo nchini Tanzania na duniani kwa ujumla, moja kwa moja kwenye barua pepe yako kutoka SportsLeo Bongo!
- ✅ Matokeo ya mechi
- ✅ Uchambuzi wa kina
- ✅ Habari za ndanii ya timu zako pendwa
✉️ Quality content, no spam. Unsubscribe anytime.