Klabu ya soka ya Yanga inatarajia kuondoka nchini siku Alhamisi kuwafuata wapinzani wao Rivers United ya Nigeria kwenye mchezo wa marejeano wa klabu bingwa Afrika hatua ya mtoano.
Yanga ilipoteza mchezo wa kwanza nyumbani kwa goli moja bila na kujiweka katika mazingira magumu zaidi itakapokuwa ugenini mwishoni mwa wiki hii.
Mmoja kati ya wajumbe wa kamati ya utendaji ya Yanga Bwana Gumbo amesema kuwa timu ipo katika hali nzuri na wanaimani kuwa watapindua matokeo hayo ugenini.
Gumbo ameelezea pia kuwa wataendelea kuwakosa wachezaji wake watatu wa kimataifa ambao ni Mayele,Aucho na Djuma Shabani kutokana na kuchelewa kwa ITC zao na pengine watajumuishwa kama Yanga watafanikiwa kufuzu hatua ya makundi.