Home Soka Yanga sc Yakamilisha Malipo ya Tambwe

Yanga sc Yakamilisha Malipo ya Tambwe

by Dennis Msotwa
0 comments

Afisa Habari wa Yanga, Hassan Bumbuli amesema tayari mshambuliaji huyo amelipwa stahiki zake zote pamoja na gharama za mawakili wake kama ilivyoelekezwa na FIFA..

“Napenda kuwathibitishia Wananchi kwamba tumemalizana na Tambwe, klabu imefanya malipo yote yaliyotakiwa kwa mujibu wa maelekezo hivyo hatudaiani chochote na Tambwe,” amesema.

Amesema Yanga imelipa jumla ya Dola za Kimarekani 22,791 ambazo ni sawa na Shilingi 52,603,000 za Kitanzania.

banner

“Kati ya pesa hizo dola 21,161 za Kimarekani ambazo ni sawa na Shilingi 48,840,900 hizi ni za deni la Tambwe na Dola 1630 ambazo ni sawa na 3,762,140 gharama za mawakili, hivyo Klabu iko huru kwenye adhabu iliyokuwa imewekwa kwenye agizo la malipo hayo,” amesema Bumbuli.

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited