Home Soka Yanga sc Yakubali Yaishe kwa Carlinhos

Yanga sc Yakubali Yaishe kwa Carlinhos

by Dennis Msotwa
0 comments

Klabu ya Yanga sc imevunja mkataba na mchezaji wake Carlos Carlinhos baada ya makubaliano ya pande mbili kuvunja mkataba huo uliokua umebakiza mwaka mmoja kumalizika.

Inasemekana hii mara ya tatu kwa kiungo huyo kuwasilisha maombi ya kuvunja mkataba na mabingwa hao mara 27 wa ligi kuu nchini lakini uongozi wa klabu hiyo ulifanikiwa kutatua migogoro hiyona kuhakikisha mchezaji huyo anakua na amani klabuni hapo.

Hata hivyo katika makubaliano ya kuvunja mkataba huo klabu ya Yanga sc imeweka vipengele kadhaa ikiwemo kulipwa kiasi cha dola laki mbili endapo atapata timu ya ndani ya nchi na pia mchezaji atalazimika kulipa asilimia 75 ya dau la usajili endapo atapata timu nje ya Tanzania.

banner

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited