Klabu ya Yanga sc imeibuka na ushindi wa bao 1-0 dhidi ya Mwadui Fc mchezo wa Ligi Kuu nchini Tanzania bara uliochezwa katika uwanja wa Kambarage mjini Shinyanga.
Bao la Yanga lilifungwa dakika ya 6 na Balama Mapinduzi kufuatia shambulizi la kushtukiza lililoanzia kwa Haruna Niyonzima kisha Jafar Mohamed aliyepiga krosi ambapo Ditram Nchimbi alikosa goli baada ya Kipa kucheza kisha mpira kumkuta Mfungaji.
Bao hilo limeweka rekodi ya kuwa bao la kwanza nchini katika mashindano rasmi tangu ligi isimamishwe siku 95 zilizopita kufuatia kusambaa kwa Virusi vya ugonjwa wa homa ya Mapafu (Covid-19).
🎯 Usipitwe!
Kuwa wa kwanza kupata habari za moto za michezo nchini Tanzania na duniani kwa ujumla, moja kwa moja kwenye barua pepe yako kutoka SportsLeo Bongo!
- ✅ Matokeo ya mechi
- ✅ Uchambuzi wa kina
- ✅ Habari za ndanii ya timu zako pendwa
✉️ Quality content, no spam. Unsubscribe anytime.
Ushindi huo Yanga imesaalia nafasi ya tatu ikiwa na pointi 54 sawa na klabu ya Azam fc japo wanatofautiana kwa tofauti ya mabao ya kushinda na kufungwa.