Home Soka Yanga yakusanya alama 3 Kagera

Yanga yakusanya alama 3 Kagera

by Dennis Msotwa
0 comments

Klabu ya soka ya Yanga imeanza vyema harakati zake za kutwaa ubingwa wa ligi kuu soka Tanzania Bara kwa ushindi wa goli 1-0 ugenini dhidi ya wenyeji Kagera Sugar katika mchezo wao wa kwanza wa ligi hiyyo.

Katika mchezo huo uliofanyika katika uwanja wa Kaitaba mjini Bukoba,Yanga ilijipatia bao lake pekee dakika ya 24 kupitia kwa nahodha wao wa leo Feisal Salum kwa shuti kali la chini akimalizia mpia uliookolewa na golikipa wa Kager Ramadhan Chalamanda.

Mabingwa hao wa kihistoria waliitwala mechi hiyo kwa kiasi kikubwa katika kipindi cha kwanza kwa pasi nyingi fupifupi na endapo wangezitumia vyema nafasi walizotengeneza basi wangeweza kufunga hata magoli matatu katika kipindi hicho.

banner

Kagera Sugar walicheza vizuri kipindi cha pili lakini shukrani kwa uimara wa mabeki Yanick Bangala na Dickson Job kambao ambao walikuwa imara kulinda lango la wanachi.

Yanga iliwakosa wachezaji wake nahodha Bakari Mwamnyeto aliyepata majeraha na Mukoko Tonombe anayetumikia adhabu ya michezo mitatu baada ya kupata kadi nyekundu kwenye fainali ya kombe la shirikisho la Azam.

Wanchi hao wanashika nafasi ya nne katika ligi hiyo wakiwa na alama tatu baada ya mchezo mmoja,msimamo kamili wa ligi kuu soka Tanzania Bara baada ya michezo ya kwanza ni kama ifuatavyo;

 

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited