Home Soka Zidane hana mpango na Man Utd

Zidane hana mpango na Man Utd

by Sports Leo
0 comments

Kocha wa zamani wa Real Madrid Zinedine Zidane hana mpango wa kuwa kocha mkuu wa Manchester United kwasasa baada ya timu hiyo kuwania saini yake kumrithi Ole Gunnar Solskjaer aliyefukuzwa kazi.

Ole alifutwa kazi siku ya Jumapili baada ya matokeo mabovu ya kufungwa 4-0 na Watford katika mchezo wa mwisho wa ligi.

Zidane hana kazi kwasasa baada ya kuachana na Madrid baada ya kumalizika kwa msimu uliopita,na kocha huyo hataki kuchukua majukumu ya ukufunzi katikati mwa msimu.

banner

Kikwazo kingine ni kocha huyo kutokuwa na uwezo wa kuzungumza lugha ya Kiingereza,kitu ambacho anafanyia kzi sasa kwa kuchukua kozi ya lugha hiyo.Hata hivyo Zidane anatamani zaidi kufanya kazi PSG kuliko kwenda Uingereza.

Man Utd kwasasa inatafuta kocha wa muda atakayeiongoza timu hiyo hadi mwisho wa msimu,huku Michael Carrick akitekeleza majukumu ya kuinoa timu hiyo muda huu ipo sokoni kumtafuta mrithi wa Ole.

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited