Home Makala Mgunda Anukia Coastal Union

Mgunda Anukia Coastal Union

by Sports Leo
0 comments

Klabu ya Coastal Union yenye makazi yake jijini Tanga imeripotiwa kuwa ipo mbioni kumrejesha kocha Juma Mgunda kuifundisha klabu hiyo baada ya kuachana nayo kumpisha Mbrazil Melis Medo.

Awali klabu hiyo msimu uliopita ilikua chini ya Mgunda ambaye alitimuliwa na kuajiriwa Mbrazil Melis Medo ambaye naye hakudumu muda mrefu na kuamua kuachia ngazi huku sababu mbalimbali zikitajwa ikiwemo kukosa maelewano na viongozi wa juu wa klabu hiyo ambapo kwa muda timu ilikua chini ya kocha msaidizi Joseph Lazaro.

Inadaiwa sasa tayari Mgunda alishakubali kurejea klabuni hapo huku akitarajiwa kuanza kazi katika mchezo wa ligi kuu dhidi ya Simba sc utakaofanyika katika uwanja wa Mkwakwani jijini humo mwezi Aprili.

banner

Mgunda ni moja ya makocha wazoefu wa Kitanzania ambapo pia amewahi kujumuishwa katika benchi la ufundi la timu ya Taifa ya Tanzania (Taifa Stars) akiwa kama mmoja ya makocha wasaidizi.

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited