Home Makala Yanga sc,Kibwana Fresh

Yanga sc,Kibwana Fresh

by Sports Leo
0 comments

Ikiwa amebakiza muda usiozidi miezi miwili  kumaliza mkataba wake katika klabu ya Yanga sc,Beki Kibwana Shomari inasemekana amekubali kusaini mkataba mpya wa miaka miwili kusalia klabuni hapo baada ya mazungumzo baina ya pande mbili kwenda sawa.

Mwakilishi wa mchezaji huyo amekutana na viongozi wa Yanga sc na kuzungumza kuhusu dili hilo la kuongeza mkataba mpya klabu hapo ambapo kwa zaidi ya asilimia tisini wamekubaliana kimsingi na imebaki kusaini mkataba mpya wa beki huyo kusalia jangwani.

Yanga sc ilimsajili Kibwana misimu msimu 2020/2021 akitokea Mtibwa Sugar baada ya kununua mkataba wake na amekua moja ya nguzo ya timu hiyo katika upande wa ulinzi wa kulia ama kushoto kutokana na mahitaji ya Mwalimu Nasreddine Nabi.

banner

Mchezaji huyo ameendelea kung’ara licha ya ujio wa Djuma Shabani katika upande wa kulia japo hakua na msimu mzuri baada ya kuwa nje ya uwanja kwa juda mrefu baada ya kufanyiwa upasuaji wa goti.

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited