Mchezaji wa klabu ya Polisi Tanzania Said Juma Makapu haonekani katika klabu hiyo tangu alipoondoka siku moja kabla ya mchezo wa ligi kuu baina ya klabu hiyo na Simba sc Klabu uliofanyika katika uwanja wa ushirika mjini Moshi.
Makapu hakuonekana katika mchezo huo ulioisha kwa sare na kusababisha Simba sc kuachwa alama 10 na watani wa jadi Yanga sc huku wakiwa na mchezo mmoja mkononi.
Kwa mujibu wa viongozi wa klabu hiyo mpaka sasa hawajui mchezaji huyo mahali alipo huku akiwa hapokei simu na wakati mwingine hapatikani kabisa japo anahitajika kuwa klabuni kwa mwajiri wake.
🎯 Usipitwe!
Kuwa wa kwanza kupata habari za moto za michezo nchini Tanzania na duniani kwa ujumla, moja kwa moja kwenye barua pepe yako kutoka SportsLeo Bongo!
- ✅ Matokeo ya mechi
- ✅ Uchambuzi wa kina
- ✅ Habari za ndanii ya timu zako pendwa
✉️ Quality content, no spam. Unsubscribe anytime.
Msemaji wa klabu hiyo inayomilikiwa na jeshi la Polisi nchini Frank Lukwaro amesema bado wanaendelea kumtafuta mchezaji huyo ili kujua zaidi sababu za kutoweka kambini.